Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Kilimo

Bodi ya Tumbaku Tanzania

Vission
Dira Yetu

Kuwa bora katika utoaji wa huduma za udhibiti, ushauri na ukuzaji wa sekta ya tumbaku.

Mission
Dhamira Yetu

Kutoa huduma kwa wakati na ubora kwa wakulima na wafanyabiashara wa tumbaku katika suala la usajili, ushauri wa kitaalam na uwezeshaji wa mchango wa sekta binafsi katika sekta ya tumbaku kwa ukuaji bora na endelevu kwa manufaa ya sekta na nchi.

Values
Tunu Zetu

  1. Ubora katika huduma
  2. Uaminifu
  3. Uadilifu
  4. Usiri
  5. Usawa

Huduma Zetu
Usajili

Bodi ina mamlaka ya kisheria ya kusajili Wakulima wa Tumbaku, Wafanyabiashara wa Tumbaku, Vyama vya Msingi vya Ushirika, Vituo vya kuchambulia na kufungia tumbaku na Vituo vya Masoko ya tumbaku. Unaweza kutembelea tovuti hii: e-Kilimo kuomba huduma hizi.

Leseni na Vibali

Bodi imepewa jukumu la kutoa leseni na vibali mbalimbali vya kuagiza na kuuza tumbaku nje ya nchi kwa wafanyabiashara wa tumbaku nchini. Baadhi ya leseni hizo ni Leseni ya Kununua Tumbaku Mbichi shambani, Leseni ya kuuza tumbaku iliyosindikwa, Leseni ya usindikaji wa tumbaku na Leseni ya kununua tumbaku iliyosindikwa. Unaweza kuomba huduma hizi kupitia tovuti ya e-Kilimo.

Huduma ya Ugani

Bodi ya Tumbaku Tanzania ina Maafisa Kilimo waliofunzwa vyema ambao hutoa utalaam, taarifa, uzoefu na teknolojia kwa wakulima wa tumbaku nchini. Ili kuhakikisha ufanisi wa tasnia ya tumbaku nchini, Bodi inatumia mafunzo na ziara za mashambani na mbinu shirikishi za ugani ili kutoa maarifa yaliyokusudiwa kwa wakulima wa tumbaku.

Bodi ya Tumbaku yatoa utaratibu wa kuomba leseni za ununuzi wa tumbaku kwa msimu wa masoko 2025/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku Tanzania Bw. Stanley N. Mnozya amewataka viongozi wote ndani ya sekta ya tumbaku kuheshimu taratibu za kilimo cha tumbaku, viongozi wa serikali na kuacha dhuruma dhidi ya wakulima wa zao la tumbaku.

Tazama jinsi Bodi ya Tumbaku Tanzania ilivyompongeza Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuibeba tasnia ndogo ya tumbaku tangu achukue madaraka ya nchi hii